• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI WANAHITAJI ELIMU ZAIDI KUHUSU COVID-19

Posted on: May 8th, 2020

Na Tegemeo Kastus

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo amewapa ndoo pamoja na sabuni za kunawa mikono maafisa Tarafa na maafisa watendaji kata wa kata zote za karatu. Zoezi hilo ni moja ya jitihada za kukabiliana na gonjwa la corona COVID-19.

Mhe. Mahongo amesema baada ya kuitisha kikao cha wadau wa afya mwezi wa tatu kujadili namna ya kupigana na janga la virusi vya corona; ikiwa ni pamoja na kuandika barua kwenye mashirika mbalimbali, Ofisi yake ilianza kupokea misaada kutoka kwa wadau. Mhe. Mahongo, amepongeza makanisa kwa kuchangia misaada mbalimbali, amesema kanisa la sabato, kanisa la Kkkt na kanisa Katoliki yametoa michango ya fedha. Mhe. Mahongo amesema vitu vingi alivyovikabidhiwa kwa maafisa Tarafa na maafisa Watendaji kata vimetoka kwa shirika la world vision.

Mhe. Mahongo amewaomba maafisa Tarafa na maafisa Watendaji kata kujikita katika kuelimisha watu juu ya ugonjwa wa virusi vya corona. Amesema kanuni za afya ni pamoja na kujali umbali wa mtu mmoja na mwingine, kuvaa barakoa na kunawa mikono kwa maji tiririka na sabauni. Amesema amepita kata ya Mang’ola akaona wananchi hawajali kuvaa barakoa kwa kisingizio ugonjwa haupo eneo lao. Ametoa maelekezo kwa Afisa Tarafa na watendaji kata kuweka mkazo katika elimu ya kuvaa barakoa.

Mhe. Mahongo amesema kwenye minada bado watu hawajahamasika kufuata kanuni za afya, ameomba maafisa hao kusimamia kikamilifu kwenye maeneo yao wakati wa shughuli za minada tahadhari zinazotolewa na wizara ya afya. Amesema kuna nchi ambazo hazijafanya lockdown lakini zinachukua tahadhari madhubuti zilizoainishwa na wataalam wa afya.

Katibu tawala wa wilaya ya Karatu Ndg. Abbas Kayanda amesema wananchi hupata huduma katika ofisi za watendaji kata na ofisi za tarafa katika maeneo yao. Amesema kwa kutambua mchango wa watendaji kata na maafisa Tarafa ni vyema watendaji hao wakajiweka katika mazingira salama katika utendaji wao wa kazi kwa kuchukua tahadhari juu ya janga la ugonjwa wa virusi vya corona.

Maafisa watendaji kata katika picha na mkuu wa wilaya Mhe. Theresia Mahongo 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2020 January 15, 2021
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2020 January 15, 2021
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • WACHIMBAJI WAASWA KUTOJIHUSISHA, UTOROSHAJI WA MADINI

    January 15, 2021
  • UMAKINI WAHITAJIKA UJENZI WA MIUNDO MBINU YA ELIMU

    January 12, 2021
  • VIJANA WAPONGEZWA, KUHITIMU MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA

    January 09, 2021
  • ARDHI NI HAKI YA KILA MTU

    December 04, 2020
  • Angalia Zote

Video

NDUGU. EDWARD MAURA MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFUGAJI NGORONGORO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0783-577 052

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa