• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

DED ATETA NA WANAFUNZI, UMITASHUMTA

Posted on: June 1st, 2021

NA TEGEMEO KASTUS

wanafunzi walioshiriki umitashumta wamefanikiwa kupata makombe sita katika michezo volleyball Mshindi wa kwanzawasichana; mshindi wa pili wavulana, mpira wa miguu mshindi wa pili wasichana, mpira wa Handball mshindi wa pili wasichana, Mshindi wa tatu wavulana na riadha mshindi wapili wa jumla na katika medali Karatu imepata medali kumi na tisa ndani yake zikiwepo medali za shaba za dhahabu na silva kulingana na ubora wa mtoto katika mashindano ya mbio.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu Ndg. Waziri Mourice amewapongeza wanafunzi hao kwa kushiriki michuano hiyo na kuleta ushindi wa makombe sita na medali. Amesema wanafunzi wamekuwa na nidhamu kubwa katika mashindano jambo ambalo limewasaidia kupata ushindi kwenye mchezo yote waliocheza.

Ndg. Waziri Mourice akipokea kombe (kulia) kutoka kwa mwanafunzi

Ndg. Waziri Mourice kama alivyoahidi hapo awali ametoa kiasi cha 390000 kama sehemu ya kupongeza kila mwanafunzi aliyeshiriki mashindano ya umitashumta. Na amewaasa wanafunzi hao kuendelea kusoma kwa bidiii ili waweze kujiunga na elimu ya sekondari na waweze kushiriki katika mashindano ya Umiseta.

Wanafunzi walioenda katika ngazi ya Mkoa kwa Halmashauri ya wilaya ya Karatu walikuwa jumla ya wanafunzi 86 huku wanafaunzi 9 wakichaguliwa kwenda kushiriki mashindano ya umitashumta kwa ngazi ya taifa. Ndg. Mourice amewapa moyo wanafunzi walioshiriki ili mwaka ujao wajipange vizuri zaidi na waweze kufanya vizuri zaidi ya walipofikia sasa.

Ndg. Waziri Mourice akizungumza na wanafunzi alipowapokea baada ya kutoka kwenye mashindano ya Umitashumta ngazi ya mkoa

Naye Afisa michezo wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu, Bi,Sara Mollel kwa niaba ya wanafunzi na walimu wa michezo amemshukuru Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya karatu kwa moyo wake wa kimichezo alioonesha wakati wa kuwaaga wanafunzi kwenda kushiriki michezo katika ngazi ya mkoa na wakati wanafunzi waliporudi kutoka kwenye michezo.

Amesema hili ni jambo la kipekeee na limeongeza hamasa na ari kwa walimu na wanafunzi ili kuhakikisha mwaka ujao wanafunzi wanafanya vizuri zaidi. Lakini amewapongeza wanafunzi kwa nidhamu walioonesha wakati wa michezo ya umitashumta, jambo ambalo limewezesha kushiriki michezo kwa amani na utulivu na kurudi nyumbani bila kupata changamoto.

Matangazo

  • WALIOCHANGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA KARATU December 14, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM PROGRAM NEW ENTRY FEE December 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA 111 NA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA 11 May 07, 2021
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MIAKA (61) YA UHURU MKUU WA WILAYA YA KARATU MHE DADI HORICE KOLIMBA AFUNGUA MDAHALO WA MAENDELEO WILAYA YA KARATU.

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM TO BE IMPROVED

    November 08, 2022
  • Angalia Zote

Video

NDUGU. EDWARD MAURA MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFUGAJI NGORONGORO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754266833

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa