• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

FEDHA MBICHI MWIBA MKALI KWA WATUMISHI

Posted on: June 11th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS

Watumishi waliotumia fedha kiasi cha 2,547,000 zilizokuwa sehemu ya ushuru wa mapato mbalimbali ya Halmashauri wamezirejesha. Watumishi hao ni bwana Mbulaingi Wali Mtendaji wa kijiji cha matala ambaye alitumia kiasi cha Tsh. 970,000. Wajumbe wa Halmashauri ya kijiji cha matala walimtaka aitishe kikao ili wasomewe mapato na matumizi ya kijiji lakini alishindwa. 

Ndg. Waziri Mourice Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri amesema hayo katika kikao cha mwisho cha baraza la madiwani. Amesema mtendaji huyo amefanya hivyo licha ya kila kijiji kufungua account benki kwa ajili ya kuweka fedha za mapato za kijiji. Amesema Mtendaji alikwepa kuitisha mkutano wa Halmashauri ya kijiji kwa sababu alitumia fedha hizo, wananchi walikasirika wakamkamata na wakamuweka ndani. Amesema baada ya kupata taarifa hizo  aliagiza Mtendaji wa kata ya Baray aambatane na askari ili wamkamate Mtendaji huyo wa kijiji na wamlete makao Makuu ya wilaya.

Amesema baaada ya kuja Makao Makuu ya wilaya  Mtumishi huyo amerudisha kiasi chote cha fedha alichotumia, Ndg. Mourice amesema bado hatua za kinidhamu zinaendelea kuchukuliwa juu yake ikiwa ni pamoja na kupangiwa majukumu mengine ya kiutumishi, amesema tayari wamemuhamisha eneo la kituo cha kazi cha matala na sasa atafanya majukumu mengine makao makuu ya Halmashauri.

Waheshimiwa madiwani wakiwa katika kikao cha baraza

Amesema kuna mtumishi mwingine Raymond Mwasha  Afisa mifugo aliyekuwa amepewa mashine ya kukusanyia mifugo na alikuwa anakusanya  ushuru wa samaki na ushuru wa sehemu ya geti la samaki. Amesema Afisa huyu alitumia fedha kiasi cha 1,577,000 kinyume na utaratibu baada ya kukamatwa na hatua za kisheria kuchukuliwa dhidi yake alirejesha kiasi hicho cha fedha.

Amesema wamemchukulia hatua za kinidhamu Afisa mtendaji huyo amesema kwa sasa hatua wanazochukua ni pamoja na kufanya ukaguzi wa mashine za ushuru (Pos) mara kwa mara. Amesema kuna wakati watendaji wanazizima (Pos) mashine za kukusanyia mapato na kupokea fedha bila kutumia mashine jambo ambalo si sawa kabisa.

Mkurugenzi ametoa rai kwa watumishi wa serikali kuona utumishi wao kama tunu na wafanye kazi kwa kufuata sheria kanuni na taratibu. Fedha ukikusanya hakikisha umeipeleka sehemu husika kuepeuka kishawishi cha kutumia; jambo amabalo ni kinyume cha utaratibu, fedha za makusanyo zinapaswa kuingizwa benki

Mkazi wa karatu Fransice Nada amesema swala la watendaji kuchukua fedha zinazokussanywa kwa ushuru ni jambo linalowaumiza wananchi. Amesema fedha hzio zinasaidia kuleta madawa vituo vya afya fedha hzio zinasaidia elimu bure hivyo watumishi kutumia fedha mbichi ni kuwaonea hasa ukizingatia wananchi waanalipa fedha ili serikali isaidie kuwaletea huduma za kijamii katika maeneo wanapoishi.

watendaji wakiwa katika kikao cha baraza la madiwani

Matangazo

  • WALIOCHANGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA KARATU December 14, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM PROGRAM NEW ENTRY FEE December 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA 111 NA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA 11 May 07, 2021
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MIAKA (61) YA UHURU MKUU WA WILAYA YA KARATU MHE DADI HORICE KOLIMBA AFUNGUA MDAHALO WA MAENDELEO WILAYA YA KARATU.

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM TO BE IMPROVED

    November 08, 2022
  • Angalia Zote

Video

NDUGU. EDWARD MAURA MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFUGAJI NGORONGORO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754266833

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa