• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

KANSAY YAPATA FEDHA ZA KUMALIZIA MRADI WA MAJI

Posted on: February 10th, 2019

Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu, Humphrey Polepole amekagua miradi ya maendeleo mbalimbali inayosimamiwa na serikali Wilayani Karatu. Mlezi huyo wa CCM mkoa wa Arusha ameomba watendaji kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua.

Ndugu, Polepole amesema hayo kwenye kikao kikuu cha Halmashauri ya CCM wilaya ya Karatu ,kilichofanyika leo katika viwanja vya ofisi ya CCM wilaya ya Karatu. Ndugu Polepole ametembelea mradi wa maji wa Kansay ambao Mhe.Rais Dkt, John Pombe Magufuli ametoa Million mia moja thelathini na tisa ambazo zitakamilisha mradi huo wa maji. Mradi huo wa maji ukikamilika utasaidia watu elfu nne wa kata ya Kansay. Fedha hizo zitatumika kusambaza mabomba kutoka mlimani na kuwafikia wananchi.

Ndugu Polepole amesema hata Mjini Karatu mradi wa Karuwasa unachangamoto. Mradi una pampu moja ya kusukuma maji, kwenye tanki lenye lita laki mbili na ishrini na tano. Uwezo wa pampu kusukuma maji kwenda mlimani ni lita elfu thelathini, na pampu inahitaji zaidi ya masaa saba ili kuweza kujaza tanki la maji mlimani. Dips za maji zikifunguliwa ndani masaa matatu maji yanakwisha, amesema watakaa kikao na Mkuu wa wilaya, watu wa Karuwasa, Waandisi wa Halmashauri na Uongozi wa Halmashauri ili iongezwe pampu ya pili Bwawani kwenye kisima cha pili ambacho hakifanyi kazi. Kisima kina uwezo wa kuzalisha maji mengine lita elfu ishirini na nane. Ambayo itakuwa imeongeza upatikanaji wa maji kwa asilimi mia moja.

Ndugu, Polepole amesema leo pia atakaa na wadau kwa ajili ya soko la Karatu ambalo lina upungufu wa millioni arobaini na tano kufanikisha upauzi wa soko. Amesema Karatu inatakiwa kutoa asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Mji mdogo lakini jambo hilo limekuwa likisua sua. Amesema fedha hizo za mapato ya ndani zinatumika kutoa mikopo ya kinamama na vijana na mikopo hiyo inapaswa iwe haina riba. Amesema baba akisafiri na mwanae basi baba anajukumu la kumlipia nauli mtoto.

Ndugu, Polepole ameahidi kutoa mkopo ya elimu ya juu kupitia Chama Cha Mapinduzi; kwa wanafunzi watakao maliza shule mwaka huu mwezi wa tano, na kufaulu vizuri kiwango cha daraja la kwanza, na lapili katika Shule ya sekondari Florian, ambayo ina wanafunzi wa kike tuu kidato cha tano na sita. Amesema yeye kama mlezi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Arusha hataki mzaha kwenye kutoa maendeleo kwa wananchi. Ndugu Polepole ameelekeza Halmashauri ya Karatu kwa miradi yote ya kimkakati ya maendeleo ambayo imekwama iletwe kwenye Chama Cha Mapinduzi.

Matangazo

  • WALIOCHANGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA KARATU December 14, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM PROGRAM NEW ENTRY FEE December 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA 111 NA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA 11 May 07, 2021
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MIAKA (61) YA UHURU MKUU WA WILAYA YA KARATU MHE DADI HORICE KOLIMBA AFUNGUA MDAHALO WA MAENDELEO WILAYA YA KARATU.

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM TO BE IMPROVED

    November 08, 2022
  • Angalia Zote

Video

NDUGU. EDWARD MAURA MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFUGAJI NGORONGORO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754266833

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa