• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

NGOMA NZITO KIKAO CHA MJI MDOGO !!!

Posted on: May 29th, 2019

Kikao cha baraza la Mamlaka ya mji mdogo wa Karatu kilichokuwa kifanyike siku ya leo kimeahirishwa kwa muda usiojulikana. Kikao hicho kilichokuwa kikiongozwa na Mwenyekiti Ndugu Elisifa Boa kimevunjika baada ya wajumbe kutaka kulipwa malimbikizo fedha zao.

Kikao hicho ambacho kilipaswa kuanza kusikilizwa saa nne asubuhi, kilichelewa kuanza  kwa mda uliopangwa. Baadae kuanza katika hali ya kuchelewa saa tano asubuhi, baada ya kufunguliwa na mwenyekiti wa Baraza la mamlaka ya mji mdogo ndugu Elisifa Boa. Mwenyekiti alianza na ajenda ya kwanza ya kufungua kikao ambayo ilifanyika kati ya ajenda nane za kikao hicho cha kawaida cha Baraza la mamlaka ya mji mdogo. Hali ilibadilika baada ya  moja ya mjumbe kuomba kupata muafaka wa fedha wanazodai kwa muda wa miezi mitatu na vikao tisa vilivyofanyika.

Ndugu Joseph Lollo amesema kwa hali jinsi ilivyo wanaanza kukosa imani na Mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo, amesema ni vyema kikao cha baraza la mamlaka ya mji mdogo kiahirishwe imefika wakati wa kupaza sauti. Baada ya hoja hizo Mwenyekiti aliwaomba wajumbe kupiga kura ili kuridhia hatua za kuahirisha kikao. Wajumbe wengi walipiga kura ya kuahirsha kikao, Mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo ndugu  Elisifa Boa alifunga kikao.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu ndugu Waziri Mourice amesema kweli amekutana na Mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo, Makamu mwenyekiti na Afisa Mtendaji mamlaka ya mji mdogo. Amesema katika kikao chao kilichofanyika Ofisi ya mkurgenzi mtendaji kuanzia mda wa saa tatu na nusu mpaka saa nne wamejadili hali ya ukusanyaji wa mapato yaliyochini ya mamlaka ya mji mdogo.

Ndugu Waziri Mourice amesema kuna kiingilio cha uwanja wa mazingira bora ambayo mpaka sasa wana 37 % tuna mwezi mmoja tu tumalize mwaka hizi asilimia zilizobakia zinakusanywa kwa utaratibu gani ? ili kutimiza malengo ya bajeti. Amesema ushuru wa taka Mamlaka wa mji mdogo kupitia wenyeviti wa mtaa wanapaswa kushirikiana na Mtendaji wa mamlaka kukusanya fedha hizo. Amesema walipaswa kukusanya million mia moja ishirini na moja laki moja na sabini na sita. Amesema mpaka sasa wamekusanya million sitini na tisa sawa na 57% kuna 43 % zinapatikana wapi ??

Ndugu Waziri Mourice amesema kuna ushuru wa nyumba za kulala wageni wamekusanya 49 % ambao ni sawa na shilingi million 36 tuu. Ndugu Waziri amehoji 51% inapatikana wapi ?? Mkurugenzi mtendaji ndugu Waziri Mourice amesema ni lazima tufanye vikao vienye ufanisi, Wenyeviti wanapaswa kushirikiana na watendaji wa Mamlaka ya mji mdogo kukusanye fedha. Ndugu waziri amesema lazima tukubali kuwajibika kufanya kazi ili tulipwe, ndugu Waziri amesema yeye anasimamia utaratibu.

Ndugu Joseph Lollo akichangia katika kikao cha kawaida cha Mamlaka ya mji Mdogo Karatu


Wajumbe wakifuatilia hoja katika kikao cha Mamlaka ya mji Mdogo

Matangazo

  • WALIOCHANGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA KARATU December 14, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM PROGRAM NEW ENTRY FEE December 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA 111 NA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA 11 May 07, 2021
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MIAKA (61) YA UHURU MKUU WA WILAYA YA KARATU MHE DADI HORICE KOLIMBA AFUNGUA MDAHALO WA MAENDELEO WILAYA YA KARATU.

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM TO BE IMPROVED

    November 08, 2022
  • Angalia Zote

Video

NDUGU. EDWARD MAURA MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFUGAJI NGORONGORO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754266833

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa