• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

NGOME YA UPINZANI KARATU YAZIDI KUYUMBA

Posted on: May 3rd, 2019

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa wa Arusha ameendelea kupokea wanachama wapya kutoka vyama vya upinzani. Ndugu  Saanare amewaapisha wanachama hao wapya na kuwapa kadi za chama cha mapinduzi wanachama zaidi ya 200 .

Miongoni mwa watu waliopokewa wapo madiwani wawili wenyeveviti vijiji vya Endagem Endabash, Ngaibara na Laja. Lakini pia chama cha mapinduzi kimepokea na kuwapa kadi wajumbe wa vijiji na wanachama wengine wapya waliojiunga na chama. Ndugu Erasto Sanare Mwenyekiti wa ccm mkoa wa Arusha  amesema amefarijika na mabadiliko wanayofanya watu wa Karatu.

 Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Karatu Ndugu Lucian Akonay amesema zaidi ya miaka 25 Karatu imekuwa haina maendeleo. Maendeleo lazima yafuate muunganiko wa ngazi za uongozi; kuanzia Mwenyekiti wa mtaa, Diwani, Mbunge na Rais, diwani pekee yake hawezi kuleta maendeleo kwa wananchi. Amesema ukichanganya viongozi wa vyama tofauti katika ngazi hizo inaleta changamoto katika utendaji wa kazi.

Ndugu Lucian amesema katika uchaguzi mdogo wa serikali za mitaa vijiji na vitongoji, ccm itafanya kampeni za kistarabu na kutoa elimu kwa wananchi. Amesema anataka viongozi watakao chaguliwa kutoa taarifa za mapato na matumizi kila baada ya  miezi mitatu. Amesema sasa ccm itafikisha madiwani 14 kutoka madiwani 4 iliyokuwa nao kwenye uchaguzi mkuu.

Mhe.Joseph Martin aliyekuwa diwani wa Oldean amesema ameunga mkono juhudi za raisi,kutokana na kazi aliyoifanya Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, amesema mambo aliyoyafanya huwezi ukalinganisha na kipindi miaka kumi iliyopita. Amesema ukitaka kujenga uchumi lazima ujitoe sadaka kwa kuchagua kilicho sahihi kwa wakati huo, ili baadae umalizie kujenga kilichobakia. Amesema huwezi kumlinganisha  Mlaji na Mzalishaji kama hujajenga miundo mbinu sahihi kama anayoifanya rais, ya kujenga standard Gauge, ujenzi wa barabara, Stigler George, kununua Ndege na kuimarisha viwanda. Wananchi sisi ni walaji na tunajihusisha na kilimo bidhaa zetu ili zifikie viwandani tunahitaji barabara nzuri reli viwanja vya ndege ili na Mlaji apate bidhaa za viwandani kama biskuti mikate kwa bei rahisi. Amesema  baadae output ya viwanda kwa maana ya faida ndio inatumika kujenga miundo mbinu ya huduma za kijamii kama hospital na shule. Amesema uchumi wa Tanzania unaimarika vizuri na Mhe. Rais Magufuli anatumia vizuri rasilimali za nchi.

Mhe. John Pissa aliyekuwa diwani wa Kansay akikabidhi kadi yake ya chama kwa Mwenyekiti wa ccm mkoa Ndugu Sanare

Mhe. Josephat Martin aliyekuwa diwani wa Oldeani akieleza sababu za yeye kujiunga na  ccm.

Matangazo

  • WALIOCHANGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA KARATU December 14, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM PROGRAM NEW ENTRY FEE December 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA 111 NA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA 11 May 07, 2021
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MIAKA (61) YA UHURU MKUU WA WILAYA YA KARATU MHE DADI HORICE KOLIMBA AFUNGUA MDAHALO WA MAENDELEO WILAYA YA KARATU.

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM TO BE IMPROVED

    November 08, 2022
  • Angalia Zote

Video

NDUGU. EDWARD MAURA MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFUGAJI NGORONGORO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754266833

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa