• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

SEKONDARI KUANZA KUFUNDISHA SOMO LA COMPUTER

Posted on: March 6th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Dunia imekuwa kijiji na hatuna budi  kuwajengea uwezo wa kitaalamu wanafunzi wa sekondari ili waweze kuendana na Mabadiliko ya sayansi na technolojia. Maudhui ya Masomo ya vitabu vya mitaala na kiada yameanza kuhifadhiwa kwenye mfumo wa (Tehama) computer unaomrahisishia mwanafunzi kupakua na kupata dondoo za masomo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda akifungua semina ya uwezeshaji ya walimu watakaofundisha somo la Tehama (computer) katika shule tisa za sekondari wilayani Karatu. Amewapongeza shirika la WEI Bantwana na SHIDEPHA kwa kusaidia kuleta somo la Tehama wilaya ya Karatu. Amesema serikali imepokea mradi huo kwa moyo mkunjufu sana, kwa sababu wamekuja kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha sekta ya elimu.

Walimu wakiwa katika semina ya uwezeshaji katika Ukumbi wa Halmashauri ya Karatu.

Walimu hao wanawezeshwa kufundisha somo la Tehama kama mitala ya elimu sekondari inayoelekezwa na wizara ya elimu. Shule ambazo zimewezeshwa walimu kupata uwezo wa kufundisha somo la Tehama ni sekondari ya Awet, Banjika, Endala, Florian, Ganako, Getamock, Mang’ola, Dkt,Wilbroad na Welwel.

Mh. Kayanda amesema kuhudhuria mafunzo ni jambo moja lakini kutekeleza maelekezo unayotakiwa kuyafuata ndio jambo la msingi. Mh. Kayanda amesema walimu wa shule hizo za sekondari tisa watambue uzito wa majukumu waliyopewa ya kwenda kufundisha wanafunzi lakini pia kuwajengea uwezo walimu wenzao katika vituo vyao vya kazi. Amesema kuwapa maarifa ya Tehama walimu wengine  kunasaidia somo hilo kuendelea kufundishwa na walimu mwingine pindi mwalimu mhusika wa somo anapokuwa hayupo.

Mh. Kayanda amesema mwalimu lazima aoneshe weledi wa kufundisha somo ili matokeo yaonekana kwa wanafaunzi na muitikio uwe mkubwa  wa kusoma na kupenda somo la Tehama.  Amesema walimu wanapaswa kumjengea mazingira mazuri mwanafunzi kulipenda somo. Wanafunzi huwa wanaelewa  masomo ya vitendo kwa sababu ni rahisi kushika na kufanyia kazi. Amesema matarajio ni kuona wanafunzi wanaopenda kusoma Tehama wanaongezeka na ufaulu wao unakuwa mzuri.

Mh. Abbas Kayanda (kushoto) akifungua semina ya walimu wa (computer) Tehama

Mh. Kayanda amesema mambo mengi sasa yanahusisha Tehama, Mathalani mfumo wa udahili wanafunzi elimu ya juu. Mwanafunzi anaomba kwenye mtandao badala ya kwenda chuo husika kuchukua fomu. Wanafunzi wanapaswa kuona somo la Tehama ni sawa na somo la kiswahili  na masomo mengine. Amesema maeneo mengine wanafunzi wanasoma somo la Tehama na kulifanyia mtihani kidato cha pili na kidato cha nne.

Naye Dkt.Herbert Mwashiuya Monitoring and Evaluation  Advisor amesema katika kusaidia kuwajengea  uwezo wanafunzi shirika la Wei Bantwana wameanzisha klabu za masomo ya Tehama. Amesema kupitia klabu za masomo mwanafunzi ataongeza udadisi zaidi na kulipenda somo la Tehama.  Amesema semina imelenga namna ya kuwajengea uwezo walimu katika kuanzisha klabu za masomo ya Tehama ili mwanafunzi aweze kurejea kujikumbusha mambo aliyofundishwa darasani kwa kupitia klabu.

Dkt. Mwashiuya amesema wakati wanaanza kutekeleza mradi wa kufundisha somo la Tehama walikuta shule za Banjika na Welwel ndio zilizokuwa zimeanza kuutekeleza mradi huo wa kufundisha somo la Tehama (Computer).

Mh. Abbas Kayanda akiwa katika picha na walimu wa (Computer) Tehama.


Matangazo

  • WALIOCHANGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA KARATU December 14, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM PROGRAM NEW ENTRY FEE December 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA 111 NA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA 11 May 07, 2021
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MIAKA (61) YA UHURU MKUU WA WILAYA YA KARATU MHE DADI HORICE KOLIMBA AFUNGUA MDAHALO WA MAENDELEO WILAYA YA KARATU.

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM TO BE IMPROVED

    November 08, 2022
  • Angalia Zote

Video

NDUGU. EDWARD MAURA MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFUGAJI NGORONGORO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754266833

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa