• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

UWEKEZAJI HEWA UKAA, NURU MPYA TARAFA YA EYASI

Posted on: November 18th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS

Kampuni ya carbon Tanzania imefanya makubaliano ya biashara ya hewa  ya ukaa na vijiji na jamii ya  Endesh, Dumechand, Jobaj, Mbuga Nyekundu,  Qangdend, Mikocheni, na Endamaghan. Mkataba huo umeandaliwa chini ya sheria ya ardhi ya vijiji na 5 ya mwaka 1999 na sheria ya mikataba ya mwaka 2002.

Akizungumza baada ya uwekaji wa saini wa mkataba huo Meneja na  muwekezaji wa kampuni ya Cabon Tanzania Ndg, David Beroff amesema wananchi  wa vijiji husika toka zamani walikuwa wanahifadhi mazingira kwa manufaa yao na wamekuwa wanatoa faida kubwa kwa dunia kutokana na uhifadhi wa mazingira.

Picha katika matukio mbalimbali wakati wa uwekaji wa sahihi wa mkataba wa kibiashara ya hewa ya ukaa kati ya muwekezaji Kampuni ya Carbon Tanzania na viongozi  wa kijiji Pamoja na jamii.

Amesema sasa ni wakati wa dunia kutambua na kuhamasisha juhudi za utunzaji wa mazingira ambazo kampuni ya Carbon Tanzania itakuwa na kazi ya kuingiza hewa ya ukaa kwenye soko la dunia. Wananchi wa vijiji husika watanufaika kwa sababu mazingira yataendelea kuwa mazuri zaidi kutokana na msukumo mkubwa watakaokuwa nao katika utunzaji wa mazingira. Amesema  wananchi wa vijiji hivyo wataweze kupata faida ya kipato kupitia serikali za vijiji husika fedha ambazo zitasaidia serikali za vijiji hivyo kuwekeza katika shughuli nyingine za maendeleo.

Afisa mazingira wa wilaya Ndg. Ally Mdangaya amesema mradi huu unahamasisha wananchi watunze mazingira katika maeneo yao. Amesema kama vijiji vitakubaliana kufuata masharti ya mkataba misitu itatunzwa na itasaidia kuongeza pato la kijiji. Ameongeza kusema kwa uzoefu ambao wamepata kwa wilaya ya jirani ya  Mbulu ambao mradi huo umeshaanza vijiji vya Tarafa ya Eyasi  vitakuwa vimepiga hatua kubwa kimaendeleo.

Mwenyekiti wa kijiji cha Endesh Ndg. Geway Namagi akizungumzia juu ya uwekaji wa saini na kampuni ya Carbon Tanzania,  amesema wanataraji kupata manufaa makubwa sana kutokana na kuwa na  maeneo makubwa ya malisho na  misitu hivyo uwekezaji huo utasaidia serikali za vijiji kuwekeza katika miradi ya maendeleo katika maeneo yao. Amesema  kazi waliyonayo sasa ni  kuhamasisha wananchi waongezee juhudi katika kuhifadhi mazingira.

Viongozi wa kijiji wakiwa katika picha ya pamoja na muwekezaji wa Kamapuni ya Carbon Tanzania

Muwekezaji huyo kampuni ya Carbon Tanzania ameingia mkataba wa miaka 20 ya uwekezaji wa hewa ya ukaa na viongozi vijiji hivyo  katika ofisi ya Afisa tarafa wa Eyasi katika zoezi lilosimamiwa na Afisa Sheria wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu.

Matangazo

  • WALIOCHANGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA KARATU December 14, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM PROGRAM NEW ENTRY FEE December 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA 111 NA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA 11 May 07, 2021
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MIAKA (61) YA UHURU MKUU WA WILAYA YA KARATU MHE DADI HORICE KOLIMBA AFUNGUA MDAHALO WA MAENDELEO WILAYA YA KARATU.

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM TO BE IMPROVED

    November 08, 2022
  • Angalia Zote

Video

NDUGU. EDWARD MAURA MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFUGAJI NGORONGORO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754266833

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa