• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WACHIMBAJI WAASWA KUTOJIHUSISHA, UTOROSHAJI WA MADINI

Posted on: January 15th, 2021

Wachimbaji na wayeyushaji wa madini ya dhahabu katika kijiji cha Endagemu maarufu kama Samunge wameaswa kutojihusisha na utoroshaji wa madini kwa sababu kufanya hivyo kunasababisha serikali kukosa mapato na takwimu sahihi zinazopatikana katika machimbo hayo ya Madini.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipotembelea machimbo ya madini pamoja timu ya wataalamu wa madini na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Karatu. Katika zaira hiyo Mkuu wa wilaya ya Karatu alipata nafasi ya kusikiliza kero za wachimbaji wa madini. Mh kayanda amesema shughuli za kuyeyusha dhahabu zinatakiwa kufanyika katika eneo la soko husika la madini ya dhahabu. Ametoa maelekezo kwa watendaji kuchukua hatua za kisheria kwa mtu yeyote atakayebainika kujihusisha na utoroshaji wa madini.

Mh. Kayanda ametembelea eneo la chanzo cha maji lilopo Katika kitongoji cha Duum katika kijiji cha Kambi ya Faru ambalo nalo shughuli za uchimbaji wa madini zianafanyika karibu na eneo la chanzo cha maji.  Mh. Kayanda amesema sheria za mazingira zinakataza shughuli zozote za kibinadamu kufanyika ndani ya chanzo cha maji ndani ya umbali wa mita 60 kutoka chanzo cha maji kilipo. Ameongeza kusema sheria za uchimbaji wa madini zinakataza kufanyika kwa shughuli zozote za uchimbaji wa madini ndani ya mita 100 kutoka eneo la chanzo cha maji.

Mkuu wa wilaya ya Karatu  Mh. Abbas Kayanda katika matukio tofauti alipotembelea wachimbaji wadogo Endagemu.

Akizungumzia  juu ya adhaa ya upatikanaji maji katika ziara  hiyo Mhandishi wa Ruwasa Injinia  Daud Ngoitanire amesema tayari ofisi yake imeshafanya  utafiti wa mwanzo na wataweka katika bajeti ya fedha  ya mwaka ujao (2021-22) ili waweze kuchimba bwawa la maji katika eneo hilo ambalo litasaidia kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa maji katika eneo la machimbo ya dhahabu Samunge.

Naye Mhandisi wa barabara wa Tarura wa wilaya Ndg. Mchele amesema changamoto za ubovu wa barabara, tayari wameshafanya uchambuzi yakinifu wa ujenzi wa barabara na swala la ujenzi wa barabara kuelekea katika machimbo hayo litawekwa katika bajeti ya barabara ya mwaka (2021-22)

Kuhusu nishati ya umeme ambayo ni moja ya changamoto kwa wachimabji hao Mhandisi wa Tanesco amesema wanampango wa kufikisha huduma za umeme katika kijiji cha Endagemu na eneo la uchimbaji litakuwa eneo lengwa.


wananchi wakimsikilza Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipofanya ziara katika Machimbo ya Endagemu (Samunge)

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa